262. BADO KITAMBO
Bado kitambo - vita itakwisha, Kitambo Na dhoruba zapoa. Na tena nitalaza kichwa changu Mbavuni mwake Anipendaye. :/:Mbinguni hazitakuwamo Dhambi, Nitaziona raha na amani.:/: Bado kitambo - roho ya umizwa, Kitambo, Kati' usiku huu. Machozi ninatoa mara Nyingi, Maana bado sijamwona Yesu. :/: Lakini asubuhi ya milele, Huko Mbinguni sitalia tena.:/: Bado kitambo cha uchovu huku, Kitambo na nitamwona Yesu, Na huru Mbali ya hatari zote, Nastarehe mikononi mwake. :/: Uvuli wote utaondolewa, Kwa Nuru huko kamilifu kweli.:/: Mateso yangu hayadhuru tena, Nitayasahau kwake Yesu, Nikisumbuka Hapa duniani, Mbinguni nitastarehe Kweli. :/: Na Mungu atafuta kila chozi, Ataondoa maumivu yote.:/: