278. NINAINUA MACHO YANGU.
Ninainua macho yangu Kwa Mungu aketiye juu,
Aliye msaada wangu, Njiani mwangu ni nuru,
Aliyefanya yote, Husikia maombi. Katika njia
Yangu yote Anilinda vema kweli.
Bwana hataniacha kamwe miguu yangu iteleze,
Yeye ndiye Mlinzi mwema, Ambaye hatasinzia.
Alinda roho yangu, Nisije kupotea, Baraka zake
Zinatosha, Kwa hitaji zangu zote.
Aniokoa na uovu, Aniponya roho yangu. Yeye
ni nguvu na wokovu, Ninahakikisha kweli.
Ananilinda pote, Kutoka na kuingia. Anijalia
mema yote, Nikimtumainia.
Comments
Post a Comment