274. NAFURAHIA KISIMA DAIMA
Nafurahia kisima daima Cha damu ya Yesu Kristo
Katika upendo nalindwa vema, Namsifu Yesu mpendwa.
Chemchemi hiyo inabubujika, Yaniletea uzima
Kando ya maji ninaburudika, Nashangilia daima.
Nakaa karibu na kisima hiki, Naishi kwa maji yake.
Yaniletea kupita kipimo, Uzima na shangwe kweli.
Nakaa karibu na kisima hiki, Naishi salama sana.
Fika upesi uliye na kiu, Kisima chabubujika!
Nakaa karibu na kisima hiki, Ni furaha na uheri.
Na kando ya maji nafasi ipo, Waweza kupona kweli.
Comments
Post a Comment