272. NI SIKU TUKUFU
Ni siku tukufu, haleluya amina,
Ya kupum-zika, haleluya, amina.
Tuache shughuli tumwabudu Mungu,
Bwana wa mbinguni, haleluya amina.
Ni siku tukufu, haleluya amina,
Tukufu kabisa, haleluya, amina.
Njoni ndugu zangu, tumwabudu Mungu,
Kwa roho na kweli, haleluya, amina.
Ni siku tukufu, haleluya, amina,
Ya furaha mno, haleluya, amina.
Yesu 'kafufuka, na sasa yu hai,
Anatuombea, haleluya, amina.
Ni siku tukufu, haleluya, amina,
Ndiyo maarufu, haleluya, amina.
Tunaye Mwokozi atuokoaye,
Sasa na milele haleluya, amina.
Ni siku tukufu, haleluya, amina,
Siku ya neema, haleluya, amina.
Tangazeni Neno la Bwana Mwokozi,
Msifuni daima, haleluya, amina.
Comments
Post a Comment