296. DHAMBI ZANGU ZIMEONDOLEWA


Dhambi zangu zimeondolewa, Mambo ya

Giza nimeyaacha. Yesu Kristo amenisafisha,

Ninamfurahia Mwokozi wangu.


Ninalo kao mbinguni Nami nimepewa vazi,

Thawabu ya ushindi ni Taji ya uzima.

Yesu ni Mwokozi wangu. Alinikomboa,

Alilipa deni langu Pendo lake kubwa nalisifu

daima, Ninamfurahisha Mkombozi.


Nimeokoka toka gizani, Zimekwisha siku

Za huzuni. Nikitapa raha na amani,

Wakati Yesu aliponikomboa.


Shaka na hofu zimeondoka, Na siogopi

Mauti tena.  Yesu Kristo ni rafiki yangu.

Kwake ninalindwa vema siku zote.


Roho wa Mungu anijaliza, Ananifariji

Safarini. Yesu Kristo yu karibu nami,

Yeye ni ngao yangu  na kimbilio.

Comments

Popular posts from this blog

264. TWENDENI, WAKRISTO

267. BABA NAKUOMBA

263. ENYI KANISA LA MUNGU