262. BADO KITAMBO
Bado kitambo - vita itakwisha, Kitambo Na dhoruba zapoa.
Na tena nitalaza kichwa changu Mbavuni mwake Anipendaye.
:/:Mbinguni hazitakuwamo Dhambi, Nitaziona raha na amani.:/:
Bado kitambo - roho ya umizwa, Kitambo, Kati' usiku huu.
Machozi ninatoa mara Nyingi, Maana bado sijamwona Yesu.
:/: Lakini asubuhi ya milele, Huko Mbinguni sitalia tena.:/:
Bado kitambo cha uchovu huku, Kitambo na nitamwona Yesu,
Na huru Mbali ya hatari zote, Nastarehe mikononi mwake.
:/: Uvuli wote utaondolewa, Kwa Nuru huko kamilifu kweli.:/:
Mateso yangu hayadhuru tena, Nitayasahau kwake Yesu,
Nikisumbuka Hapa duniani, Mbinguni nitastarehe Kweli.
:/: Na Mungu atafuta kila chozi, Ataondoa maumivu yote.:/:
Comments
Post a Comment