285. SOMA BIBLIA

 

Soma Biblia, chuo cha wokovu, Tulichopewa

na Mungu Baba. Biblia inatuambia kweli:

Njoo kwa Yesu Mwokozi wetu!


Chunguza neno tulilopewa, Linatuonyesha

njia ya kweli, Nuru gizani ya kutuongoza

Katika mwendo kwenda Mbinguni.


Soma Biblia, giza linakuja Kama

walivyosema manabii. Biblia yetu

yatuangazia Kutuonya  njia hata mwisho.


Katika neno la Biblia yetu Tunapewa

utajiri wote. Mbingu na nchi

zitaangamia, Neno la Mungu halitapita.

Comments

Popular posts from this blog

264. TWENDENI, WAKRISTO

267. BABA NAKUOMBA

263. ENYI KANISA LA MUNGU