284. TUMESOMA MENGI


Tumesoma mengi juu ya Bwana Yesu

Upendo wake, ishara zake. Na usome tena,

Ukamwombe Mungu, Na utaona maajabu.


Hata leo yanatokea, Tunapoomba kwa imani.

Tuombe tu, Atusikia, Na tuatona maajabu.


Jamaa ya Naini wakosa amani,

Wafadhaika, Wahuzunika. Bali Bwana

Yesu 'kafanya ajabu. Aliyekufa 'kahuika.


Ahadi ya Mungu, Roho mtakatifu,

Ilitimizwa Yerusalemu. Walikutanika,

Roho akashuka, Kwa lugha mpya wakamsifu.


Petro kahutubu, wengi wakatubu,

wakagairi Dhambi za siri, Waliopokea

Neno lake Bwana Wakabatizwa siku ile.


Nilimwomba Yesu, Nikapata nguvu,

Na jambo hili ni la fadhili, Nilisamehewa

Dhambi zikafutwa, Nimeupokea wokovu.

Comments

Popular posts from this blog

264. TWENDENI, WAKRISTO

267. BABA NAKUOMBA

263. ENYI KANISA LA MUNGU