275. EE MUNGU MWENYE HAKI


Ee Mungu mwenye haki, niongoze huku Katika

mambo yote yakupendezayo. Bila wewe,

Bwana Yesu, mashaka mengi ninayo Ya

kunitisha hapa safarini mwangu.


Kumtegemea Yesu ni heri daima, na kutembea

naye kwa kila hatua, Kwa kuwa yeye ni

Mchunga. Ananiongoza vema, Nipate kuingia

kwake mbinguni juu.


Nina safari sasa ya kwenda mbinguni.

Mwokozi yuko huko, Lazima nifike. Na siku ya

kuingia Nitashangilia kweli Kumwona na kum-sifu

Mwokozi wangu.


Ulimwenguni huku kuna shida nyingi,

Nikihitaji kitu, ninahangaika. Lakini siku ile kuu

nitakapomwona Yesu, Natumiani  sitaikosa Thawabu.


Mbinguni sitaona uovu wowote. Wala kukuta

Mambo ya huzuni tena. Sauti nitamtolea

kusema: "Ee, Mungu mwema!" Mikono

nitaipepea kwa shangwe kuu.

Comments

Popular posts from this blog

264. TWENDENI, WAKRISTO

267. BABA NAKUOMBA

263. ENYI KANISA LA MUNGU